Tuesday 2 December 2014

JINSI YA KUTENGENEZA MAZIWA YA CHUPA YA UNGA KWA MTOTO MCHANGA (FORMULA MILK)



Kinga hasili (immunity) ya kichanga chako sio imara kama ya mtu mzima, hivyo vichanga huweza kupata maambukizi ama malazi upesi kuliko mtu mzima. ii inamaanisha usafi ni muhimu sana sana wakati wa kumtengenezea kichanga chakula.

Vyombo vyote vinavyotumika kutengenezena chakula cha mtoto vinatakiwa viwe sterile (Yaani viwe kwenye hali ambayo haina wadudu). Hivyo basi chupa, chuchu ya chupa, mfuniko wa chupa na vyote vya kumwandalia mtoto vioshwe na kusterelize kila kabla ya kuvitumia kumlisha mtoto ili kupunguza chance ya mtoto kupata maambukizi ya magonjwa kama kuharisha.

Wadudu wa Bacteria kwenye maziwa ya unga 

Ingawa maziwa ya unga huwa yamefunikwa na kuzibwa kabisa (sealed), yanaweza pia kuwa na bacteria ndani kama Cronobacter sakazakii na mara chache huwa na salmonella. Ingawa case kama hizi hutokea mara chache lakini maambukizi yake ni ya hatari sana kwa kichanga na yanaweza sababisha mauti.


Bacterial huzaliana kwa upesi sana kwenye joto la kawaida la ndani ya nyumba (room temperature), hata kama maziwa yataachwa kwenye fridge bado hawatakufa na wataendelea kuzaliana ingawa baridi upunguza kasi ya kuzaliana.

Ili kupunguza maambukizi, ni vizuri kutengeneza maziwa mara moja pale tuu mtoto anapoyahitaji. k/a*ti
Tumia maji ya kunywa ya bomba yaliyochemshwa, Usitumie maji yalichemshwa zamani. Ukishachemsha maji yaache yapoe kwa mda wa dakika 30 na sio zaidi ndipo uyatumie kutengeneza maziwa. Hii itahakikisha kwamba joto la maji bado halipungui 70C. Maji katika joto hili litaua wadudu wa maambukizi kama bacteria. Kumbukuka kuacha maziwa yaendelee kupoa kabla ya kumpatia mtotot anywe.

Usitumie maji ya chupa ya dukani kutengeneza maziwa 

Maji ya kununua dukani hayashauriwi sababu kwanza sio sterile alafu pia yanaweza kuwa na kiasi kikubwa cha chumvi (Sodium) ama Salphate unles kiwe si zaidi ya 200mg. Ikiwa ni lazima utumie maji ya dukani basi hakikisha unayachemsha pia.

Matengenezo


  • Chemsha maji ya bomba (usitumie ambayo yamechemshwa zamani)
  • Yaache yapoe kwa dakika 30 tuu ili joto lisipungue chini ya 70C.
  • Safisha eneo unalotumia kutayariashia maziwa
  • Ni muimu sana kunawa mikono yako
  • Tumia sterelizer kusterelise chupa za mtoto, ama kama hauna chemsha vyupa vya maziwa.
  • Tafadhari hakikisha unapochemsha ama kusterelise vyupa hakikisha unaifungua chupa yote yaani unatoa vifunuko, chuchu na kuvichemsha vyote pamoja.
  • Weka chuchu na kifuniko vikiangalia juu na sehemu safi
  • Fuata maelekezo ya kwenye kopo la maziwa jinsi ya kutengeneza, angalia level ya maji, anza kujaza maji kwenye chupa kwanza wakati yakiwa bado yamoto kabla ya kumimina maziwa.
  • Unapojaza maziwa kwenye kijiko hakikisha kiasi hakiwi kama kimlima ( kiwe flat) tumia kisu kama inawezekana.
  • Changanya maziwa mpaka poda isionekane.
  • Yaache yapoe zaidi ili mtoto asiungue wakati akinyonya.
  • Test joto la maziwa kwa kumimina kido kwenye kiganja cha mkono.
  • Maziwa yakibaki baad ya kunyonya yamwage.
  • Tafadhari usitumie microwave kupasha moto maziwa yanaweza kumuunguza mtoto.












No comments:

Post a Comment