Tuesday 11 June 2013

Mtoto miezi 6 mpaka 12


Rudi mtoto chini ya miezi 6

Mtoto miezi 6 mpaka 12

Mpaka wa 6, mtoto anaweza kulala muda wa masaa 3 wakati wa mchana na kulala zaidi ya masaa 9 hadi 11 wakati wa usiku. Katika umri huu, unaweza kumuacha alie usiku, hii ni kwa watoto wachanga ambao huamka na kulia wakati wa usiku.

Wazazi wanaweza kuwapatia watoto muda kidogo watulie na kujirudisha kulala wao wenyewe bila kubembelezwa. Kama huwezi kumwacha mwanao akilia basi mbembeleze bila kumbeba kwa kumuongelesha akiwa kitandani huku unamsugua (rub) mgongoni kidogokidogo, alafu muache uondoke akijua kwamba anatakiwa kurudi kulala - isipokuwa kama anonekana kuwa mgonjwa. Watoto wagonjwa wana haja ya kubebwa na kutunzwa. Kama mtoto wako haionekani mgonjwa na anaendelea kulia, unaweza kusubiri kwa muda mrefu kidogo, kisha rudia tena kumwacha ajibembeleze yeye mwenyewe atakapolia tena.

Kati ya miezi 6 na 12, wasiwasi wa kutengana toka kwa mama humpata mtoto, hii ni kawaida na ni sehemu ya ukuaji ya mtoto. Sheria ni ileile, jaribu kutombeba mtoto wako, kutomwashia taa, kutomwimbia, kutomwongelesha, kutocheza nae, au kulisha mtoto wako wakati anatakiwa alale. Hizi zote hazitamruhusu mtoto wako kujifunza kulala mwenyewe na ataendelea kuamka usiku.

Watoto chini ya miaka 3
Kuanzia mwaka 1 hadi 3, wengi wachanga kulala masaa 10 hadi 13. Kujitenga wasiwasi, au tu hamu ya kuwa pembeni na mama na baba (ili asimiss kitu), inaweza kuwahamasisha mtoto kukaa macho.

Wazazi wakati mwingine kufanya makosa ya kufikiri kwamba kumwacha mtoto asilale mapema kutamfanya mtoto alale zaidi usiku. Kiukweli, ingawa, watoto wanaweza kuwa na wakati mgumu kulala kama wamechoka sana. Ingawa watoto hulala kidogo mchana, usimlazimishe alale mchana kama hataki, lakini ni muhimu kuwa na ratiba ya muda wa utulivu kwa mtoto, akae chumbani kwa mda hata kama kataki kulala mchana.

Kuanzisha utaratibu wa kwenda kulala husaidia watoto kupumzika na kuwa tayari kwa ajili ya usingizi. Kwa mtoto, utaratibu unaweza kuwa toka dakika 15 hadi 30 na ni pamoja na shughuli za kutulia kama vile kusoma hadithi, kuoga, na kusikiliza muziki laini.

Chochote utakachofanya, mwanao anatakiwa ajue ni usiku na anatakiwa alale, usibadilishe mpangilio ulouweka kila siku kabla ya kulala.  Kila inapowezekana, mruhusu mwanao achague nini anataka usiku huo, yaani kama ni hadithi, ama kuimbiwa, nguo  gani ya kulalia anataka, toy ipi ya kulala nayo anataka, nyimbo iipi, hadithi ipi n,k ilimradi bado mtafuata mpangilio uleule kila siku. Hii inamfanya anaona ana udhibiti kwenye huu mpangilio.

Lakini hata mtoto mlalaji  huwa anaamka mara moja moja. Kuota meno kunaweza  kumuamsha pia ndoto. Ndoto huanza katika umri huu, na kwa watoto wadogo, ndoto inaweza kuwa ni kutisha. Jinamizi ni hasa inatisha kwa watoto, ambao hawawezi kutofautisha mawazo na ukweli. (Basi kuwa makini kuchagua programu gani mwanao anaangalia  kabla ya kwenda kulala)


Kuwafariji na kushikilia mtoto wako kwa nyakati hizi. Kuwa na majadiliano juu ya ndoto kama yeye anataka, na kukaa hadi mtoto wako ni atulie. Kisha muhimize mtoto wako arudi kulala mapema iwezekanavyo.

No comments:

Post a Comment