Wednesday 8 June 2011

Mimba Wiki ya 3 na ya 4

Mwili wako

Hongera, inawezekana bado hujui lakini una mimba. Ingawa hauhisi chochote bado mwili wako tayari unafanya kazi kwa kasi kujiandaa kwa ajili ya miezi tisa ijayo.

Nini Kinafanyika ndani ya kizazi(Uterus)

Kizazi kawaida kina uzito wa 60g na 7.5cm kwa urefu, Lakini pindi tuu uzazi unapotunga kinaongezeka kwa ajili ya uongezefu wa hormone inayoitwa oestrogen ambayo inatolewa na placenta. Hormone hii ni muhimu kwani ndio inayo saidia kutengenezwa na kukuza kwa mtoto tumboni, viungo kama mapafu, maini, kidney n.k havitakomaa pasipo hii hormone. Uzazi unanenepa na kusababisha layer kubwa ya majimaji ambayo ndipo mtoto atakapoishi na kukua kwa kipindi chote cha ujauzito. kipindi hichohicho muscle fibers zinajijenga kujiandaa kuzaliwa kwa mtoto.


Nini kinafanyika kwenye shingo ya uzazi (Cervix)

Shingo inaongezeka kidogo kwa upana, inarainika na rangi yake kuwa nyeusi zaidi kuliko kawaida sababu ya kuongezeka kwa uwingi wa mishipa ya damu kwenye eneo hilo. Glands kwenye cervix inajenga ute mzito (Mucus plug) kugundisha shingo ya kizazi ili kisipatwe na maradhi kumkinga mtoto akiwa tumboni.

Kwa kipidi hichi chote hautoona hedhi mpaka ujifungue.