Tuesday 16 April 2013

Unawezaje kupata mtoto wa kike?



Haya wanduguuu, wataalamu wanasema kwamba huwezi kuamua ni mtoto gani unayemtaka kabla ya kuconceive. Hii inatokana na kwamba hujui kama kwenye mbegu ya kiume ni chromosome X ama chromosome Y ndio iliogelea kwa kasi zaidi kuliko yenzake. Mimi binafsi nina vidume viwili na ningependa kweliii nipate wa kike. Hivyo basi nimeamua ku-dig nikapata mawili matatu, eti wanasema kuna njia (Ambazo nitajaribu) ambazo zinaweza kumsaidia X awe mjanja ama Y kuwa mjanja. Lakini kwa leo nitagusia jinsi gani ya kumsaidia X kuwa mjanja.

Mbegu ya mwanaume ina chromosomes mbili, Y na X, mbegu hii ina kiwango sawa cha X na Y (50/50). Y inapo-conceive ndipo unakuwa na mtoto wa kiume na X inaposhinda unapata mtoto wa kike. Ingawa Y anaonekana mjanja na mwepesi kuliko X, haina nguvu kama X. Kujua hili inasaidia kupanga jinsi ya kumpata mtoto wa kike, hii ndio silaha yako.  Y kutokuwa na nguvu kunamaanisha kwamba Y anakufa upesi kuliko X, hivyo basi fanya ufanyavyo kuhakikisha kwamba Y anakufa ili ubakiwe na X tuu.

Pangilia mda mzuri wa kupata mtoto wa kike: Y-chromosome ina haraka lakini haiishi zaidi ya siku tatu na X chromosome haina haraka lakini huishi mpaka siku tano. Hivyo basi jaribu ku-conceive siku tatu kabla ya ovulation yako ianze. Ila, ukishafanya mapenzi hiyo siku ya tatu kabla ya ovulation kuanza hutakiwi kufanya tena mpaka ovulation iishe. Hii inatokana na sababu ifuatayo: Unapofanya mapenzi siku tatu kabla ya ovulation, zile mbegu za kiume zenye X na Y zinaanza kuogelea na kupigania kwenda kwenye yai la mwanamke lakini mbegu ya mwanamme haito-conceive sababu ovulation kwa mama inaanza baada ya siku tatu, yaani mbegu za mwanamme zimeingia mapema (During the safe days) kabla ya ovulation. Kwa sababu Y chromosome haiishi zaidi ya siku tatu, basi siku ya tatu pindi ovulation kwa mama inapoanza tayari Y chromosome zitakuwa zimeshakufa na mbegu za mwanaume zitakuwa imebakiwa na X chromosomes tuu. Hivyo basi unajipatia chance kubwa ya kuwa na mtoto wa kike.

Ili hii plan ifanye kazi, unatakiwa uwe na uhakika siku yako unapoanza ovulation (yaani kipindi unachoweza kushika mimba). Labda umeshasikia kwamba ovulation inaweza anza kuanzia siku ya 14 ya mzunguko wako ingawa hii inatofautiana tofautiana. Kuna njia nyingi ya kujua lini unaovulate, dalili za kuonyesha ovulation angalaia hapa. Kuna vifaa ambavyo vinasaidia ku-predict ovulation yako, vinaitwa "Ovulation test kits", vinavyotumia saliva ni vizuri zaidi kuliko za mkojo kwani unaweza kurudia kutumia mara nyingine.

10 x Ovulation Test Kits  Accurate Ovulation Prediction Test Cassettes Muonekano wa Ovulation kits

Position wakati wa mapenzi:

Jaribu kufanya mapenzi kwenye position ambayo ni vigumu kwa mbegu za kiume kujipenyeza ndani, hii ili kuzipatia kazi ngumu ya kulifikia yai la kike. Positions hizi ni kama zifuatazo:

 Spooning Position:                                           Traditionary missionary position



                               

                          
PH ya mwili:  Mwili ukiwa na acid nyingi inasaidia kuua chromosome Y upesi. Kama nilivyosema hapo mwanzo Y haina nguvu, hivyo kwenye mazingira ya acid inakufa upesi. Hivyo basi unashauliwa kula vyakula vyenye kiasi kikubwa cha acid. Vyakula hivi ni kama: apples, blueberries, cherries, grapes, grapefruit, nectarines, peaches, pears, pineapple, plums, raspberries. Kuna recipe ya kukupatia acid nyingi mwilini kama hivi. Pia kuna njia nyingine ya kuongeza mazingira ya acid kwenye sehemu ya mwanamke, hii ni kuyakalia maji ya acid (kama maji ya vinegal) kabla ya kufanya mapenzi. 

Kwa ufupi tuu, ukichanganya njia zote tatu utakuwa na chance kubwa ya kupata mtoto wa kike (90%).

Nitawajulisha kama nitafanikiwa, all the best my dears na good luck kwa kutafuta mtoto wa kike.
                           







PH ya mwili




No comments:

Post a Comment