Tuesday 2 December 2014

Kutapika na Kuharisha kwa watoto

Ni kawaida kwa watoto wachanga na watoto kutapika. Katika kesi nyingi , kutapika hudumu kati ya siku moja mpaka mbili na si ishara ya kitu chochote kikubwa . Kawaida sababu ya kutapika kwa watoto ni gastroenteritis . Haya ni maambukizi ya kolomeo kawaida husababishwa na virusi au bakteria. Na pia husababisha kuhara . Mfumo wa kinga ya mtoto wako kwa kawaida hupigana na maambukizi baada ya siku chache.

Watoto mara nyingi pia hutapika wakati wanapomeza  hewa wakati wa kulishwa . Hata hivyo , kuendelea kutapika wakati mwingine inaweza kuwa ni ishara ya kitu kibaya zaidi , ikiwa ni pamoja maambukizi makali kama vile uti wa mgongo.

Ukurasa huu unaeleza nini cha kufanya kama mtoto wako anaendelea kutapika na iuaelezea baadhi ya sababu ya kawaida ya kutapika kwa watoto wachanga, na watoto kwa ujumla . Kama mtoto wako ana joto la juu , unaweza pia kusoma kuhusu homa kwa watoto

Nini cha kufanya.

Kama mtoto wako anatapika, unapaswa kufuatilia hali kwa uangalifu mkubwa. Amini moyo wako na mpeleke kwa dakitari wako mara moja kama wewe una wasiwasi.

Kama sababu ni tummy bug tuu (kuhara kwa kawaida kwa mtoto ama tummy flu), atakula na kucheza kama kawaida.  Katika kesi hiyo, endelea kumlisha kama kawaida na kumpatia kinywaji (maji, juice n.k) mara kwa mara. Maji humsaidia kutopunguka kwa uwingi wa maji mwilini ambao ni hatari.

Lakini kama haonekani  wa kawaida, - kwa mfano, kama yupo floppy , hasira , kutojibu, au amepoteza hamu ya kula -  inawezekana anaumwa, hivyo unapaswa kuwasiliana na daktari wako mara moja.


Kumpeleka kwa daktari

Unapaswa kuwasiliana na daktari wako kama :

          •Mtoto wako amekuwa akitapika kwa zaidi ya masaa 24
          • Mtoto wako  anatapika  ndani ya masaa nane, au kama unafikiri amepungukiwa na
            maji mwilini.
          • Kama ni floppy, mwnye  hasira, anagoma chakula , au hayupo kwenye hali ya kawaida
,         • Ana maumivu makali tummy
          • Ana maumivu ya kichwa na shingo ngumu.

Ishara ya upungufu wa maji mwilini
Kutapika  kali na kuhara kunaweza kwa urahisi kusababisha upungufu wa maji mwilini , hasa katika
watoto wachanga. Hii ina maana mwili wa mtoto wako hana maji ya kutosha mwilini  au hana chumvi inayohitajika kwa ajili ya mwili kufanya kazi kwa kawaida .

Watoto wenye upungufu wa maji  mara nyingi hujisikia na huonekana kuumwa.

 Ishara ya upungufu wa maji mwilini ni :
• kinywa kikavu
• kilio bila kutoa machozi
• kukojoa kidogo sana au kiasi cha nappies anazokojolea kupunguka.
• Kuongezeka kwa kiu
• Kudhoofika

Ufanyaje

Jambo muhimu zaidi unaweza kufanya kama mtoto wako anatapika ni kuhakikisha anaendelea kunywa maji ya kunywa.
Kama mtoto wako anatapika , endelea kumnyonyesha. Kama wamepungukiwa maji, , atakuwa anahitaji maji ya ziada. Uliza mfamasia wako kama wangeweza kupendekeza kumpatia dawa ya kusaidia kutopunguka kwa maji mwilini.
Dawa hii ni poda maalum unaitengeneza kwa kuweka kwenye maji. Ina sukari na chumvi katika kiasi maalum ya kusaidia kuchukua nafasi ya maji na chumvi kupotea kwa njia ya kutapika na kuhara.
Watoto ambao hutapika wanapaswa kunywa maji haya kidogokidogo hivyo hawatapungukiwa maji
mwilini. .Pia motto anaweza kunywa maji , maji mengi kwenye juice ya kuchanganya na maji , diluted maji ya matunda au maziwa.
Hata hivyo, kama pia wanaharisha, maji ya matunda  ziepukwe. Tena, GP wako au mfamasia anaweza kupendekeza ORS.


Dawa ya kusaidia wakati wa kuharisha kwa motto.


Sababu ya kutapika kwa watoto.
 Kuna sababu ya uwezekano wa kutapika katika watoto, ambayo ni ilivyoelezwa hapo chini


  •  gastroenteritis
    Gastroenteritis ni maambukizi ya utumbo. Ni kitu cha kawaida inayosababisha kutapika kwa watoto na kwa kawaida huchukua muda wa siku chache .
  • maambukizo ya hatari
    Watoto wadogo hasawapo  katika hatari ya kupatwa na maambukizi kama vile pneumonia au maambukizi ya figo. Unapaswa kuwasiliana na daktari wako kama motto ana dalili ya magonjwa haya.
  • ugonjwa wa kidole tumbo
    Ugonjwa wa kidole tumbo










JINSI YA KUTENGENEZA MAZIWA YA CHUPA YA UNGA KWA MTOTO MCHANGA (FORMULA MILK)



Kinga hasili (immunity) ya kichanga chako sio imara kama ya mtu mzima, hivyo vichanga huweza kupata maambukizi ama malazi upesi kuliko mtu mzima. ii inamaanisha usafi ni muhimu sana sana wakati wa kumtengenezea kichanga chakula.

Vyombo vyote vinavyotumika kutengenezena chakula cha mtoto vinatakiwa viwe sterile (Yaani viwe kwenye hali ambayo haina wadudu). Hivyo basi chupa, chuchu ya chupa, mfuniko wa chupa na vyote vya kumwandalia mtoto vioshwe na kusterelize kila kabla ya kuvitumia kumlisha mtoto ili kupunguza chance ya mtoto kupata maambukizi ya magonjwa kama kuharisha.

Wadudu wa Bacteria kwenye maziwa ya unga 

Ingawa maziwa ya unga huwa yamefunikwa na kuzibwa kabisa (sealed), yanaweza pia kuwa na bacteria ndani kama Cronobacter sakazakii na mara chache huwa na salmonella. Ingawa case kama hizi hutokea mara chache lakini maambukizi yake ni ya hatari sana kwa kichanga na yanaweza sababisha mauti.


Bacterial huzaliana kwa upesi sana kwenye joto la kawaida la ndani ya nyumba (room temperature), hata kama maziwa yataachwa kwenye fridge bado hawatakufa na wataendelea kuzaliana ingawa baridi upunguza kasi ya kuzaliana.

Ili kupunguza maambukizi, ni vizuri kutengeneza maziwa mara moja pale tuu mtoto anapoyahitaji. k/a*ti
Tumia maji ya kunywa ya bomba yaliyochemshwa, Usitumie maji yalichemshwa zamani. Ukishachemsha maji yaache yapoe kwa mda wa dakika 30 na sio zaidi ndipo uyatumie kutengeneza maziwa. Hii itahakikisha kwamba joto la maji bado halipungui 70C. Maji katika joto hili litaua wadudu wa maambukizi kama bacteria. Kumbukuka kuacha maziwa yaendelee kupoa kabla ya kumpatia mtotot anywe.

Usitumie maji ya chupa ya dukani kutengeneza maziwa 

Maji ya kununua dukani hayashauriwi sababu kwanza sio sterile alafu pia yanaweza kuwa na kiasi kikubwa cha chumvi (Sodium) ama Salphate unles kiwe si zaidi ya 200mg. Ikiwa ni lazima utumie maji ya dukani basi hakikisha unayachemsha pia.

Matengenezo


  • Chemsha maji ya bomba (usitumie ambayo yamechemshwa zamani)
  • Yaache yapoe kwa dakika 30 tuu ili joto lisipungue chini ya 70C.
  • Safisha eneo unalotumia kutayariashia maziwa
  • Ni muimu sana kunawa mikono yako
  • Tumia sterelizer kusterelise chupa za mtoto, ama kama hauna chemsha vyupa vya maziwa.
  • Tafadhari hakikisha unapochemsha ama kusterelise vyupa hakikisha unaifungua chupa yote yaani unatoa vifunuko, chuchu na kuvichemsha vyote pamoja.
  • Weka chuchu na kifuniko vikiangalia juu na sehemu safi
  • Fuata maelekezo ya kwenye kopo la maziwa jinsi ya kutengeneza, angalia level ya maji, anza kujaza maji kwenye chupa kwanza wakati yakiwa bado yamoto kabla ya kumimina maziwa.
  • Unapojaza maziwa kwenye kijiko hakikisha kiasi hakiwi kama kimlima ( kiwe flat) tumia kisu kama inawezekana.
  • Changanya maziwa mpaka poda isionekane.
  • Yaache yapoe zaidi ili mtoto asiungue wakati akinyonya.
  • Test joto la maziwa kwa kumimina kido kwenye kiganja cha mkono.
  • Maziwa yakibaki baad ya kunyonya yamwage.
  • Tafadhari usitumie microwave kupasha moto maziwa yanaweza kumuunguza mtoto.