Tuesday 11 June 2013

Mtoto kutolala usiku

Je mwanao huwa ana tabia ya kuamka usiku? 
Huwa anakufuata chumbani kwako?
Anataka kulala pembeni yako?

Watoto wanapokuwa wachanga huwa wananyonya maziwa ya mama ama ya chupa kila baada ya masaa machache. Hivyo mazoea ya kuamka usiku kwa ajili ya kunyonya huwa yanaendelea pindi mtoto huyo anapokuwa na umri wa kuweza kulala usiku bila kutegemea chakula. Hii huwa inatokana na mzazi/wazazi kuiendeleza iyo tabia kwa kumpatia mtoto maziwa usiku. mtoto pindi anapoanza kuanza kula chakula kigumu         basi unaweza kuanza kumtoa kwenye kunyonya usiku polepole mpaka ataweza kulala mwenyewe usiku mzima bila kuamka.

Kama unataka kurekebisha hiyo tabia unaweza kufanya yafuatayo:

Kiasi gani cha usingizi kinatosha kwa mwanao?

hii inategemea na umri wa mtoto na mtoto mwenyewe. Watoto wapo tofauti, Hermes anaweza kulala toka saa 2.00 usku mpaka saa 2 asubuhi, wakati Henrick yeye ni mtoto wa maluelue analala atalala kuanzia saa 3 usiku na kuamka saa 12 asubuhi. utamjua mwanao kama ana usingizi/anakosa usingizi mara tabia zake zikichange, anaweza kuwa juu juu, mbishi na analialia.  hizi chini ni masaa ya kulala kwa mtoto kutegemeana na umri wake:

Watoto chini ya miezi 6

Hakuna formula ya kulala kwa ajili ya watoto wachanga  kwa sababu saa zao mwilini hazijakamilka bado. Wao kwa ujumla huwa wanalala au drowse kwa masaa 16 hadi 20 kwa siku, hii ni kati ya usiku na mchana.

Watoto wachanga lazima waamshwe kila baada ya masaa 3 na 4 hadi uzito wao uwe imara, ambapo kwa kawaida hutokea ndani ya kipindi cha wiki moja. Baada ya hapo ni sawa kama mtoto akilala kwa muda mrefu zaidi.
Baada ya wiki chache za mwanzo, watoto wachanga wanaweza kulala kwa muda mrefu kama masaa 4 au 5  huu ndio muda ambao matumbo yao madogo yanaweza kumudu kati ya ulishaji. Kama watoto hulala vizuri wakati wa usiku, basi watakula zaidi wakati wa mchana.

Wakati tu wazazi wanapohisi kuwa kulala usiku kunaonekana kama ndoto ya mbali, usingizi wa mtoto wao kawaida huanza kuhama kuelekea usiku. Anapokuwa na miezi 3, mtoto hulala kwa wastani wa masaa 13 katika kipindi cha saa 24 (yale masaa 4-5 ya kulala wakati wa mchana  huvunjwa katika kulala mara mojamoja(naps) na masaa 8-9 wakati wa usiku. Asilmia 90% ya watoto wa umri huu hulala usiku mzima, kwa maana ya masaa 5 hadi 6 katika mfululizo.

Lakini ni muhimu kutambua kuwa watoto hawawi macho saa zote, wakati wanasikika kama wapo macho, wao wanaweza kulia na kufanya kila aina ya kelele nyingine wakati wa usingizi wa mang'amung'amu. Hata kama wakiamka usiku, wanaweza tu kuwa macho kwa dakika chache kabla ya kurudi tena kulala wao wenyewe bila kubembelezwa. 

Kama mtoto chini ya umri wa miezi 6 anaendelea kulia, ni vizuri kwenda kumsikiliza. Mtoto wako inawezekana kuna kitu kinachomfanya alie, njaa, joto, amekojoa, baridi, au hata mgonjwa. Lakini mara kwa mara usiku kumuhudumia mtoto usiku kwa ajili ya kumbadilisha na kumlisha lazima iwe ya haraka na kimyakimya. Kipindi hiki usifanye chochote kile kitakachomwamsha mtoto kama kuzungumza, kucheza, au kuwasha taa. Muhimiza kwamba ni usiku na ni kwa ajili ya kulala. Unamfundisha hili kwa sababu mtoto wako hajali ni muda gani ilimradi mahitaji yake yanakamilishwa.

Kimsingi, mtoto wako lazima awekwa kwenye kitanda kabla ya kuanza kusinzia. Na si mapema mno kuanzisha kamchezo cha kwenda kulala mda fulani kila siku, unaweza kumzoesha kumwimbia kabla ya kilala, fanya mfululizo na katika utaratibu huo kila usiku.

Lengo ni kuwafanya watoto walale kwa kujitegemea, na kujifunza kujibembeleza wenyewe na kurudi kulala pindi wanapoamka usiku wa manane.

Angalia mtoto miezi 6 mpaka 12







No comments:

Post a Comment