Je mwanao
huwa ana tabia ya kuamka usiku?
Huwa anakufuata chumbani kwako?
Anataka kulala pembeni yako?
Watoto wanapokuwa wachanga huwa wananyonya maziwa ya mama
ama ya chupa kila baada ya masaa machache. Hivyo mazoea ya kuamka usiku kwa
ajili ya kunyonya huwa yanaendelea pindi mtoto huyo anapokuwa na umri wa kuweza
kulala usiku bila kutegemea chakula. Hii huwa inatokana na mzazi/wazazi
kuiendeleza iyo tabia kwa kumpatia mtoto maziwa usiku. mtoto pindi anapoanza
kuanza kula chakula kigumu basi unaweza kuanza
kumtoa kwenye kunyonya usiku polepole mpaka ataweza kulala mwenyewe usiku mzima
bila kuamka.
Kiasi gani cha usingizi kinatosha kwa mwanao?
hii inategemea na umri wa mtoto na mtoto mwenyewe. Watoto
wapo tofauti, Hermes anaweza kulala toka saa 2.00 usku mpaka saa 2 asubuhi,
wakati Henrick yeye ni mtoto wa maluelue analala atalala kuanzia saa 3 usiku na
kuamka saa 12 asubuhi. utamjua mwanao kama ana
usingizi/anakosa usingizi mara tabia zake zikichange, anaweza kuwa juu juu,
mbishi na analialia. hizi chini ni masaa ya kulala kwa mtoto kutegemeana
na umri wake:
Watoto chini ya miezi 6
Hakuna
formula ya kulala kwa ajili ya watoto wachanga kwa sababu saa zao mwilini
hazijakamilka bado. Wao kwa ujumla huwa wanalala au drowse kwa masaa 16 hadi 20
kwa siku, hii ni kati ya usiku na mchana.
Watoto
wachanga lazima waamshwe kila baada ya masaa 3 na 4 hadi uzito wao uwe imara,
ambapo kwa kawaida hutokea ndani ya kipindi cha wiki moja. Baada ya hapo ni
sawa kama mtoto
akilala kwa muda mrefu zaidi.
Baada
ya wiki chache za mwanzo, watoto wachanga wanaweza kulala kwa muda mrefu kama
masaa 4 au 5 huu ndio muda ambao matumbo yao madogo yanaweza kumudu kati ya
ulishaji. Kama watoto
hulala vizuri wakati wa usiku, basi watakula zaidi wakati wa mchana.
Wakati
tu wazazi wanapohisi kuwa kulala usiku kunaonekana kama ndoto
ya mbali, usingizi wa mtoto wao kawaida huanza kuhama kuelekea usiku. Anapokuwa
na miezi 3, mtoto hulala kwa wastani wa masaa 13 katika kipindi cha saa 24
(yale masaa 4-5 ya kulala wakati wa mchana huvunjwa katika kulala mara mojamoja(naps)
na masaa 8-9 wakati wa usiku. Asilmia 90% ya watoto wa umri huu hulala usiku
mzima, kwa maana ya masaa 5 hadi 6 katika mfululizo.
Lakini
ni muhimu kutambua kuwa watoto hawawi macho saa zote, wakati wanasikika kama wapo macho, wao wanaweza kulia na kufanya kila
aina ya kelele nyingine wakati wa usingizi wa mang'amung'amu. Hata kama
wakiamka usiku, wanaweza tu kuwa macho kwa dakika chache kabla ya kurudi tena
kulala wao wenyewe bila kubembelezwa.
Kimsingi,
mtoto wako lazima awekwa kwenye kitanda kabla ya kuanza kusinzia. Na si mapema
mno kuanzisha kamchezo cha kwenda kulala mda fulani kila siku, unaweza
kumzoesha kumwimbia kabla ya kilala, fanya mfululizo na katika utaratibu huo
kila usiku.
Lengo
ni kuwafanya watoto walale kwa kujitegemea, na kujifunza kujibembeleza wenyewe
na kurudi kulala pindi wanapoamka usiku wa manane.
Angalia mtoto miezi 6 mpaka 12
Angalia mtoto miezi 6 mpaka 12
No comments:
Post a Comment