Tuesday 30 September 2014

Ugonjwa wa vipele kutokana na nappy za kutupa (mapampas)

Leo nimeona tujulishane na kubadilishana mawazo kuhusu hili suala la allergy ya diapers (tunayaita mapapas) kwa watoto wetu. Kutokana na mabadiliko ya kimaendeleo siku hizi sio kama zamani watotot wetu yumezowea kuwavalisha chupi/ nappy za kutupa, yaani zikishajaa mikojo hatufui tena badala yake unazitupa.

Vipele kutokana na diapers ni kawaida kwa watoto na sio ishara ya kumtelekeza mtoto. Huu ni ugonjwa wa ngozi amba unatokana na kugusana na kitu ambacho husababisha allergy na matokeo yake vipele hutokea. Angalia picha zifuatazo:

Huu ugonjwa husababishwa na bacteria ama fangasi ambao kwa kawaida huwepo kwenye ngozi ya mtoto.

Kumbadilish mtoto diaper mara kwa mara inasaidia kupunguza vichochezi kwa allergy hii.  Vichochezi huwepo kwenye ngozi ya mtoto.

Mtoto anapokuwa na ugonjwa huu jitahidi kuacha kutumia baadhi ya mafuta ama creams ambazo zisizopitisha hewa kuingia kwenye ngozi (mfano, petrolium jelly, mafuta ya mgando ya kupaka) na wakati mwingine antifungal cream, low-potency hydrocortisone cream. High-potency steroid creams, powders, na baking-soda/boric-acid baths and neomycin-containing ointmentspia ni za kuziepuka.












 Nini husababisha vipele vya diaper

Kuna makundi kadhaa ya sababu wa ugonjwa huu wa ngozi Kwanza kabisa ni "kikereketa" au "kugusana(contact)"  Ngozi huonekana nyekundu (kama vile imechomwa na jua) alafu hubadilika na kuwa na tabaka (layer) juu wa ngozi. Tofauti ya ugojwa huu na magonjwa mengine ya ngozi ni kwamba utagundua kutokuwepo kwa vipele sehemu zenye mikunjo kwenye ngozi ya mtoto (matakoni), hii inaonyesha kwamba mkojo na kinyesi huchangia kwani mikojo na kinyesi huwa na wadudud wa bacteria na fungus. Mikojo na kinyesi huwa hazifiki sehemu zenye mikunjo na ndio maana hakuna wadudu hawa, hivyo vipele huwa havionekani sehemu hizi

Bacteria aina ya (Staph na Strep) na fungus aina ya candida mara nyingi ndio huonekana kwenye ugonjwa wa diaper. Kama imesababishwa na bacteria basi huanza kwa kusababisha vipele vidogodogo (Impetigo) ambavyo huja kuwa malengelenge na kupasuka na kujisambaza, matakoni na sehemu za karibu,  hii husababisha  kuwashwa kwa ngozi.

Kama imesababishwa na fungus basi huoneka ngozi madoa madoa  myekundu na ukubwa (kati ya 2mm - 4mm). Mara nyingi huonekana karibu na sehemu ya kutolea haja kubwa. 

Ugonjwa huu ni rahisi kuujua kwa macho tuu, ukiwa na tatizo mpeleke mtoto kwa daktari. 

Vikereketa mara nyingi hutokana na harufu na material ya diaper. Ingawa ni mara chache sana allergy ndio sababu ya ugonjwa huu, lakini kama ukiona tatizo ni diaper basi badilisha diper. Pia ikiwezekana jaribu kutumia wipes zisizo na harufu.

Tufanyeje?


Dawa kubwa ni kuzuia mtoto asipate huu ugonjwa, nimelist vitu vya kufanya kama ifuatavyi:

1. Wewe kama mzazi (mama ama baba) unatakiwa kumkagua mtoto kila siku, nasema hivi sababu wazazi wengi huwaachia mabinti wa kazi kulea mtoto na  hujisahau majukumu yao kama wazazi. Hi itasaidia kuona kama ugonjwa huu unapoanza.

2. Jitahidi kumuogesha mtoto asubuhi na kabla hajaenda kulala, hii mara nyingi husaidia safisha kikereketa ambacho kilibaki kwenye diaper (ikiwezekana msafishe mtoto na maji kila unapombadilisha diaper badala ya kutumia wipes) Wipes zitumike pale ambapo maji hakuna.

3. Upele unapotokea, msafishe na maji na nguo safi na laini na sio wipes. 


Kwa maelezo zaidi tembelea zifuatazo

Hapa na hapa