Ni kawaida kabisa kutokwa na majimaji mazito (vaginal
discharge) ukeni wakati ukiwa na ujazito.
Usiwe na wasiwasi kama majimaji haya ni myepesi na yana muonekano wa
rangi ya maziwa.
Dalili za kuwa na
fungus ukeni:
·
Majimaji yakiwa mazito, myeupe na rangi ya
maziwa, na yanayoonekana kama cottage cheese, ama maziwa ya mgando, ama
yaliyoharibika.
·
Kama unawashwa, na kusikia kuvimba kama vile
umejikwaruza, na muonekano wa uwekundu sehemu ya ukeni.
·
Inauma wakati wa kujamiiana
·
Unasikia kuchomwachomwa wakati unakojoa
Je nilipataje thrush:
Maambukizi ya ukeni wakati wa mimba ni ya kawaida. Thrush
husababishwa na fungus (yeast) wanaoitwa
candida albicans ambao wapo na huishi kwenye miili yetu bila kusababisha tatizo
lolote. Wapo pia kwenye mfumo wa chakula na mara nyingi hawana madhara yoyote
kwetu na wala hautojua kama wapo.
Huwa wanaleta tatizo pale tuu wakati fungus hawa na vijidudu
vingine ndani na nje ya mwili vinapopungua ama kuongezeka kuliko kiasi
kinachitakiwa. Unaweza kupata thrush
pale ambapo:
·
Unapokuwa mjamzito mabadiliko ya hormones kwenye mwili
husababisha mwili uwe na sukari nyingi kuliko kiasi inayoitwa glycogen
ambayo husababisha fungus kuzaliana kwa wingi (wanatumia glycogen kama chakula
na hivyo kuwapatia nguvu ya kujiongeza idadi).
·
Unapotumia antibiotics, dawa hizi huua vijidudu
mwilini ambapo pia huua vijidudu vizuri vinavyopigana na vile vibaya, hivyo
basi balance ya vijidudu hivi inakuwa imebadilika na hiyo kusabaisha vile
vibaya vizaliane kwa nguvu.
·
Kisukari (Diabetes): kama una ugonjwa wa kisukari
ambacho huujakicontrol pia husababisha thrush.
·
Kama immune system yako ni dhoofu. Hii inaweza
kutokana na pia na matibabu ya magonjwa kama sarakani (cancer) ama magojwa na
HIV.
Ingawa thrush sio magonjwa ya zinaa, yanawezekana
kuambukizwa kama partner wako amepata maambukizi haya, hivyo mnashauriwa wote
wawili mpate matibabu kwa wakati moja.
Kama unafikiria una thrush, tafadhari mwone daktari.
Daktari atakupatia dawa, ingawa wanashauri kutotumia
chochote kipindi cha mlongo wa kwanza wa mimba (miezi 3 ya mwanzo) .
Dawa zingine ni za kuweka ukeni (kidonge), unashauriwa
kuweka usiku wakati umelala ili inyonywe vizuri wakati umelala. Thrush ni
vigumu kupona upesi hivyo basi ni vyema umalize dozi utakayopewa na
daktari. Tafadhari usichukue dawa za
vidonge ambayo utahitaji kumeza, bado haijajulikana kama vina madhara gani kwa mtoto.
Je nifanyeje
·
Wakati unapojiosha ukeni, usitumie sabuni osha
na maji masafi (sio ya kisima) ikiwezekana jichemshia maji kidogo tuu(kuua
vijidudu) kwa ajili ukeni. Na ikiwezekana jioshe mara moja kwa siku kwani
kujisafisha sana ukeni unaondoa wale wadudu wanaohitajika kulinda uke (Good
Flora microorganism).
·
Usitumie mafuta yatakayoirritate ngozi kama pedi
za kunukia, deodorant za ukeni, na sabuni zakunukia.
·
Kula maziwa mgando yasiyo na sukari, ama ingiza
maziwa ya mgando ukeni.
·
Kama utatumia maziwa mgando, njia rahisi ya
kuweka ukeni ni kwa kutumia tampoo, chovya tampoo kwenye maziwa mgando,
dumbukiza tampoo ukeni, iache kwa muda wa lisaa limoja, alafu itoe.
·
Kupunguza kueneza thrush, basi jifute toka mbele
kwenda nyuma kila baada ya kutumia choo.
·
Vaa chupi za cotton 100%
·
Wakati wa kujamiiana tumia kilainisho(lubricant)
kupunguza maumivu kama una thrush.
Je thrush itamfikia
mtoto tumboni
Hapana, mtoto amefunikwa na mfuko na hatadhurika.
Hata hivyo ni muhimu kupata matibabu kabla ya kujifungua,
kwani mtoto anaweza kuambukizwa wakati akitokea ukeni.
Kama hii ikitokea basi utahitaji matibabu wewe na mtoto,
mtoto mara nyingi anakuwa na utando mweupe kwenye ulimi.
Utagundua thrush huja na kuondoka wakati wa mimba, na huchukua
mda mrefu kuitibu lakini sio kitu cha kuogopa sana.
Dah! Nashukuru sana mke wangu ana tatizo hili na linaogopesha sana lkn kwa elimu yako nimefarijika. Ubarikiwe sana doctor.
ReplyDeleteAsanteee docta me hii hali napitia nimepewa dawa lkn hali imerudi vilevile,, nifanyaaje?
ReplyDeleteJeee. Haiathiri afya ya mtoyo
ReplyDelete